Rais Kikwte azindua Jengo la Mahakama ya Mwanzo Rondo,Lindi vijijini
Jundu(kushoto),Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Bernard Membe(watatu kulia) na mkuu wa mkoa wa Lindi Ludovick
Mwananzila wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa jengo la Mahakama ya
Mwanzo lilijengwa kwa nguvu za wananchi na wafadhili katika kata ya
Rondo,jimbo la Mtama,Lindi vijijini jana.
HAFLA YA MIAKA 20 YA CLUB BILICANAS NA MIAKA 13 YA CLOUDS FM YAFANYIKA
Keki iliyoandaliwa kwa ajili ya hafla hiyo
………………………………………………….
Na Andrew Chale
WADAU mbalimbali wa burudani
usiku wa kuamkia jana walifurahia kwa pamoja na kula keki ya miaka 20
ya klabu ya Kimataifa ya Bilicanas na miaka 13, ya Clouds Fm,
iliyoambatana na shamrashamra mbalimbali ndani na nje ya ukumbi huo.
Sherehe hizo ziliongozwa na
Mkurugenzi Mtendaji wa Bilicanas Group, Dk. Lilian Mtei ambapo
aliwashukuru wadau hao kwa kuwa bega kwa bega na klabu hiyo, tangu 1992.
“Tunawashukuru sana kwa kuwa nanyi mara zote inatia faraja kwetu na
tutaendelea kutoa huduma bora siku zote|” alisema Mbowe.
Mtei pia aliwashukuru
wafanyakazi mbalimbali waliofanikisha ukumbi huo kufikia hapo na kutoa
heshima ya kipekee kwa wafanyakazi waliokuwapo tokea inaanza hadi
ilipofikia miaka 20 na hatimaye kukata keki hiyo.
“Uwepo wa miaka 20, tuna kila
sababu ya kuwapongeza wafanyakazi tuliokuwa nao toka mwanzo hadi leo,
na kwa heshima ya pekee Mama Victor na Mrs Mitemo ndiyo watakao kata
keki hii” alisema Mtei.
Keki hiyo ilikatwa na
wafanyakazi hao Monica Victor na Pili Mitemo ambaye alimwakilisha
mumewe aliyekuwa Meneja wa kwanza wa klabu hiyo, ambaye kwa sasa ni
marehemu.
Aidha, kwa upande Clouds FM,
iliwakilishwa na Wasiwasi Mwabulambo ambaye alipongeza klabu Bilicanas
kwa kuwa mstari wa mbele katika kuinua sanaa nchini hasa kwa kuwasaidia
wasaidia wasanii kufikia malengo yao.
Kwa upande wake Ibrahim Tuwa
‘Dj Ibra’ aliyekuwa akisherehesha shughuli hiyo, aliwaomba wadau
kuendelea kuwaunga mkono na wataendelea na huduma bora zaidi ha hapo. Dj
Ibra alijiunga na Bilicanas tokea 2002,ambapo mpaka sasa ana miaka 10
kwenye klabu hiyo iliyowahi kuwa na madj maarufu waliopita hapo ambao
wengi wao wapo kwenye vituo vya televisheni na redio.
No comments:
Post a Comment